Monday 29 June 2009

USA 2-3 Brazil !!
Brazil abeba Kombe la Mabara!
Nini Makocha wamesema baada ya mechi?
USA waliongoza 2-0 hadi kipindi cha kwanza kumalizika lakini Brazil walipachika bao 3 kipindi cha pili na kutwaa Kombe la Mabara.
Kocha wa USA Bob Bradley amesema: ‘Kufungwa kunatuumiza sana! Nasikia fahari juu ya Wachezaji wangu lakini tunajisikia vibaya kuacha ushindi ukituponyoka! Nadhani dunia nzima sasa watagundua tuna Timu nzuri na Wachezaji wazuri!’
Kocha wa Brazil Dunga anatamba: ‘Hata baada ya kuwa 2-0 nyuma, Timu ilikuwa na uhakika! Hafutaimu tuliwaambia wacheze kwa kutumia Wingi na wawe wavulimivu! Tulifanya hivyo, tuko pamoja siku 29 sasa na tulilitaka sana Kombe hili!’
Kaka atwaa Mpira wa Dhahabu!! Mpira wa Fedha na Kiatu cha Dhahabu chabebwa na Luis Fabiano!!!
Wakati Timu yao imenyakua Kombe la Mabara, Wachezaji wawili wa Brazil wamepata Tuzo za juu za Mashindano haya na nao ni Kaka aliyetunukiwa Mpira wa Dhahabu wa Adidas na Luis Fabiano aliyeshinda Tuzo mbili, moja ikiwa ni Mpira wa Fedha na Kiatu cha Dhahabu kwa kuwa Mfungaji Bora wa Kombe la Mabara kwa kufunga bao 5.
Mpira wa Shaba ulichukuliwa na Clint Dempsey wa USA, Kiatu cha Fedha kimebebwa na Fernando Torres wa Spain kwa kufunga bao 3 na Kiatu cha Shaba kapewa David Villa wa Spain.
Kipa Bora wa Mashindano hayo ameteuliwa kuwa Tim Howard wa USA na amezawadiwa Glovu za Dhahabu.
Timu Bora ni Brazil na imetunukiwa Tuzo ya Uchezaji wa Haki na FIFA.

No comments:

Powered By Blogger