Sunday 28 June 2009

KOMBE LA MABARA: Mechi ya Mshindi wa 3: Afrika Kusini 2 Spain 3!!!
SPAIN WATWAA USHINDI WA 3!!!!
Katika mechi iliyokwisha dakika chache zilizopita, Wenyeji Afrika Kusini, wakiwa Uwanjani Royal Bafokeng huko Rustenrburg, walitangulia kupata bao dakika ya 77 kupitia Mphela lakini ndani ya dakika moja Spain waliweza kusawazisha na kupachika la pili, mabao yaliyofungwa na Guiza dakika ya 88 na 89.
Hata hivyo Afrika Kusini waliweza kusawazisha kwenye dakika za majeruhi pale Mphela tena alipofunga kwa frikiki na kuifanya gemu iwe 2-2 na kuingizwa kwenye dakika 30 za nyongeza.
Robo saa ya Kipindi cha kwanza cha nyongeza kilikwisha huku mechi ikibaki 2-2.
Dakika 2 tu baada ya Kipindi cha Pili cha Nyongeza kuanza, Spain wakapachika la 3 kupitia Alonso aliefunga kwa frikiki na hivyo kuwafanya Spain kuwa Washindi wa 3 wa Kombe la Mabara.

Fainali itakayoanza baadae leo kati ya USA na Brazil itatoa Bingwa na Mshindi wa pili.
VIKOSI:
SPAIN: CASILLAS, ALBIOL, VILLA, TORRES, CAPDEVILA, SERGIO, ALONSO, RIERA, ARBELOA, CAZORLA.
AFRIKA KUSINI: KHUNE, GAXA, MASILELA, MOKOENA, SIBAYA, TSHABALALA, PIENAAR, MODISE, DIKGACOI, BOOTH, PARKER
REFA: MATTHEW BREEZE [AUSTRALIA]

No comments:

Powered By Blogger