Friday 3 July 2009

REAL: BADO MTU MBILI!!!
Rais wa Real Madrid, Emmanuel Perez, amesema bado wanahitaji kusaini Wacheza wawili zaidi ili kukamilisha ujenzi wa Kikosi kipya huko Santiago Bernabeu.
Tayari Real Madrid, wakimwaga vijisenti kichizi, wameshawateka Cristiano Ronaldo, Kaka na Raul Albiol kwa jumla ya dau la ajabu la Pauni Milioni 148 na sasa wako njiani kumshika Karim Benzema kutoka Lyon ya Ufaransa.
Perez hakutaja ni Wachezaji gani watawabeba ingawa Kiungo wa Liverpool Xabi Alonso amehusishwa sana na pia Franck Ribery wa Bayern Munich ambae Klabu yake ya Bayern Munich haitaki aondoke.

No comments:

Powered By Blogger