Wednesday 1 July 2009

Brazil yaing’oa Spain, sasa ni NAMBARI WANI Duniani!!!
Bongo tuko Topu Mia!!!
Baada ya kunyakua Kombe la Mabara huko Afrika Kusini Jumapili iliyopita, Brazil wamechukua Nambari Wani kwenye Listi ya FIFA ya Nchi Bora Kisoka Duniani na kuidondosha Spain hadi nafasi ya pili.
Kwa mara ya mwisho Brazil kuwa kileleni ni Agosti mwaka 2007.
Timu ya 3 ni Uholanzi, 4 ni Italia na Ujerumani ni nafasi ya 5.

Nafasi ya 6 ni Urusi, England ni wa 7 na Argentina wa 8.
Timu ya juu kabisa toka Afrika ni Ivory Coast walio nafasi ya 18 wakifuatiwa na Cameroun nafasi ya 29, Gabon ya 30, Nigeria ya 34, Ghana 35 na Misri ya 38.
Timu yetu, Bongo, tuko nafasi ya 97 tukiwa tumezipita Gambia ambao wako nafasi ya 99, Congo DR nafasi ya 102, Angola 103, Kenya 105, Malawi 110, Rwanda 113, Namibia 115, Zimbabwe 116.
Timu ya mwisho kabisa kwenye listi hiyo ya FIFA ni Papua New Guinea walio nafasi ya 203.

No comments:

Powered By Blogger