Thursday 2 July 2009

NI YALE YALE: Ribery ni Real tu!!!!
Franck Ribéry, aliehusishwa kwenda Chelsea au Manchester United, ametoka bayana na kusema anataka kwenda Real Madrid na si kwingineko.
Hii inafuatia uthibitisho kuwa Mchezaji mwenzake wa Ufaransa, Karim Benzema, yuko safarini kuelekea Real.
Pia, kauli ya Ribery inatoa ushahidi mkubwa kuwa huwezi kumchukua Mchezaji yeyote wa Ufaransa endapo Real Madrid inamtaka kwa sababu tu upo mkono mkubwa wa Zinedine Zidane anae warubuni Wachezaji hao kwa sababu ni Balozi wa Real Madrid.
Hata hivyo, Klabu ya Franck Ribery, Bayern Munich ya Ujerumani ambayo Ribery alijiunga 2007 akitokea Marseille ya Ufaransa, imetoa msimamo wao kupitia Meneja Mkuu Uli Hoeness ambae ameshangaa: ‘Ni kweli Franck anataka kwenda Real? Kwa sisi, hiyo haibadilishi kitu! Maisha siku zote si ndoto tamu! Real hawajaongea chochote na sisi hatuhitaji pesa zao!’

No comments:

Powered By Blogger