Sunday 28 June 2009

Barcelona yatoboa Man City imetoa ofa kubwa kumnunua Eto’o!!!
Rais wa Barcelona Joan Laporta amepasua kuwa Manchester City wametoa ofa ya dau ‘kubwa sana’ kumnunua Samuel Eto’o.
Eto’o, Mchezaji wa Kimataifa toka Cameroun mwenye umri wa miaka 28, amebakiza mwaka mmoja tu kwenye mkataba wake na Barcelona na inasadikiwa atahama.
Ingawa Eto’o hataki kuhama Barcelona lakini inaaminika dau na malupulupu atakayopewa na Man City yatamfanya ashindwe kukataa ofa hiyo.
Laporta anasema: ‘Eto’o hataki kuondoka lakini ofa kama hii huwezi kuikataa!’
AC Milan yathibitisha kumtaka Adebayor!!!
Makamu wa Rais wa AC Milan Adriano Galliani amethibitisha kuwa Klabu yake ambao ni Vigogo wa Serie A huko Italia wana nia ya kumnunua Emmanuel Adebayor kutoka Arsenal.
Baada ya kumuuza Kaka kwenda Real Madrid, AC Milan wana kitita cha kumnunua Adebayor ingawa inaaminika nia yao hasa ni kumchukua Edin Dzeko kutoka Wolfsburg ya Ujerumani.
Dzeko ni raia wa Bosnia.
Galliani amethibitisha ameshazungumza na Meneja wa Arsenal Arsene Wenger kuhusu Adebayor.

LEO FAINALI KOMBE LA MABARA: USA v BRAZIL huko Bondeni!!!
Kocha wa Brazil, Dunga, haamini kuwa kile kipigo cha 3-0 walichowapa USA huko Bondeni wiki iliyopita kwenye mechi za Makundi kwenye Kombe hili la Mabara kina maana yeyote kwenye Fainali ya leo ambayo Brazil wanakutana tena na Marekani Uwanja wa Ellis Park huko Johannesburg, Afrika Kusini katika mechi ya Fainali itakayoanza saa 3 na nusu, bongo taimu.
Hata alipoambiwa kuwa katika mechi 15 Brazil walizocheza na USA, ni mara moja tu USA walishinda na Brazil kushinda mara 14, Dunga alitamka: ‘Soka si historia, haihusu yaliyopita au mapya yatakayokuja!’
Falsafa ya Dunga inamwonyesha ni mtu wa aina gani, yaani mtu makini mwenye mpangilio wa nini muhimu!
Kwa yeye kitu muhimu ni Fainali ya leo na wala si ule ushindi wa bao 3-0 walipowapiga USA huko Tshwane, Pretoria siku 10 zilizopita.
Dunga anasema: ‘Ushindi ule umepita! Lazima uiheshimu Timu ambayo baada ya kufungwa mechi 2 wakaibuka na kuwafunga Misri na Spain! Wana nidhamu kwenye mbinu zao na wakakamavu dakika zote 90!’
Dunga akiongelea Timu yake amesema: ‘Hii ni gemu ambayo lazima tuwe na uwiano kati ya defensi na mashambulizi. Nimejifunza miaka mingi kuwa kama timu haina uwiano huo, haifiki mbali! Ni lazima tuwe na Wachezaji wapiganaji pale kati wanaosaidia defensi, kunyang’anya mipira na kulisha fowadi. Kule Brazil huwa tunawaita hawa Wapiga Piano. Ndio maana kwenye mtindo wetu Gilberto Silva na Felipe Melo ni muhimu sana! Wao wanahenya ili kuwapa mwanya wataalam wetu, Wachezaji wenye vipaji wawe huru kucheza soka lao!’

No comments:

Powered By Blogger