Saturday 27 June 2009

FAINALI Jumapili 28 Juni 2009: USA v Brazil
UWANJA: ELLIS PARK, JOHANNESBURG SAA: 3.30 USIKU [Bongo Taimu]
USA itabidi wachezeshe Kiungo mwingine badala ya Michael Bradley ambae alipewa Kadi Nyekundu katika Nusu Fainali waliyoibwaga Spain 2-0.

Benny Felhaber anategemewa kuchukua nafasi yake.
Brazil, mbali ya Juan ambae ni majeruhi, hawana tatizo kwa Mchezaji mwingine yeyote.
Hii ni mara ya pili kwa Timu hizi kucheza kwenye Kombe hili huko Afrika Kusini kwani walikuwa Kundi moja na Brazil aliichapa USA 3-0 kwa magoli yaliyofungwa na Felipe Melo, Robinho na Maicon.
Mpaka sasa Brazil na USA zishacheza mara 15 na Brazil kushinda mara 14 na USA kushinda mara moja tu na hiyo ilikuwa mwaka 1998 walipoifunga Brazil 1-0 huko Los Angeles.
VIKOSI VINATEGEMEWA KUWA:
USA:
Howard; Spector, Onyewu, DeMerit, Bocanegra ,Dempsey, Felhaber, Clark, Donovan, Davies , Altidore
Brazil: Cesar; Maicon,Lucio, Luisao, Santos Melo, G Silva, Ramires, Kaka, Fabiano, Robinho.
Refa: M Hansson (Sweden).

No comments:

Powered By Blogger