Saturday 27 June 2009

VIJANA CHINI MIAKA 21 ULAYA: England yaingia Fainali kwa Matuta!
England 3 Sweden 3
Baada ya kutoka suluhu 3-3, England iliwabwaga Wenyeji Sweden kwa mikwaju ya penalti 5-4 na kuingia Fainali watakapokutana na Germany walioifunga Italia 1-0.
Fainali hiyo itachezwa Jumatatu.
Mpaka mapumziko, England ilikuwa mbele kwa mabao 3-2 yaliyofungwa na Martin Cranie, Onuoha na la tatu Mattias Bjarsmyr wa Sweden alijifunga mwenyewe.
Kipindi cha pili Sweden wakarudisha bao zote 3 kupitia Ola Toivonen na Marcus Beg aliefunga 2.
Frazier Campbel, Kijana wa Manchester United, ataikosa Fainali baada ya kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu kufuatia Kadi 2 za Njano.
Kipa Joe Hart wa Manchester City nae ataikosa Fainali kwa kupewa Kadi ya Njano wakati wa kupigiana penalti kwa kosa la kuvuka mstari wa goli.

No comments:

Powered By Blogger