Wednesday 24 June 2009

KOMBE LA MABARA HUKO BONDENI: Nusu Fainali kati ya Spain na USA!!!
Wengi hawakupinga kutinga kwa Spain Nusu Fainali lakini ni wachache mno ndio waliootea USA itatinga Nusu Fainali hasa baada ya kubamizwa katika mechi zao mbili za kwanza kwenye Kundi lao. Lakini wametinga Nusu Fainali baada ya kuwafunga Mabingwa wa Afrika, Misri, mabao 3-0 katika mechi yao ya mwisho Kundini huku Mabingwa wa Dunia, Italia, wakipigwa 3-0 na Brazil.
Mechi ya leo, inayoanza saa 3 na nusu usiku saa za bongo, inaikutanisha Spain, Mabingwa wa Ulaya na Nambari Wani Duniani katika listi ya FIFA, ambayo haijawahi kufungwa na USA.
Beki wa Spain, Gerard Pique wa Barcelona ambae pia aliichezea Manchester United, ametamka: ‘Ni ngumu kila mtu akikuona unastahili kushinda mechi na itabidi kufanya kazi ya ziada kuingia Fainali!’
Nae Kocha wa USA, Bob Bradley, anasema: ‘Tulicheza na Spain kabla ya EURO 2008 na tulicheza vizuri tu! Tumewatazama wanavyocheza na tunajua staili yao! Tunajua namna ya kuwasimamisha na tunajiamini!’

Refa wa mechi hii ni Jorge Larrionda kutoka Uruguay.
UEFA U21 CUP: Nusu Fainali ni England v Sweden na Italy v German siku ya Ijumaa
Wenyeji Sweden jana walidunda Nusu Fainali ya Kombe la UEFA la Vijana wa Chini ya Miaka 21 walipoifunga Serbia 3-1 mjini Malmo, Sweden na sasa watakutana na England siku ya Ijumaa.
Katika mechi nyingine ya Kundi A, Italia waliipiga Belarus 2-1 na pia kutinga Nusu Fainali watakayocheza na Germany pia siku ya Ijumaa.
Washindi watakutana Fainali Jumatatu tarehe 29 Juni 2009 kupata Bingwa wa Ulaya wa Timu za Taifa za Vijana wa chini ya miaka 21.
LIGI KUU……………….kwa ufupi:
Birmingham………………………..
Kipa Joe Hart wa Manchester City amepelekwa Birmingham kucheza kwa mkopo msimu ujao na mwenyewe ameonyesha masikitiko yake kwa uamuzi huo.
Joe Hart kwa sasa yuko na Kikosi cha England cha Vijana wa chini ya miaka 21 huko Sweden wakigombea Ubingwa wa Ulaya.
Hart amenena kwa masikitiko: ‘Si kitu nnachopenda, navumilia tu lakini si mwisho wa dunia!’
Klabu hiyo mpya ya Kipa Joe Hart, Birmingham iliyopanda Daraja kuingia Ligi Kuu, imemsaini Mchezaji wa Kimataifa wa Ecuador Giovanny Espinoza kutoka Klabu ya Barcelona Sporting Club ya Ecuador.
Beki huyo wa Kati, aliechezea mechi 80 kwenye Timu ya Taifa ya Ecuador na ambae ameshacheza Fainali za Kombe la Dunia mara 2, amesaini mkataba wa miaka wawili.
Kwa Meneja wa Birmingham, Alex McLeish, huyu ni Mchezaji wa 5 kumsaini kwa msimu ujao wengine wakiwa Christian Benitez, Scott Dann, Stephen Carr na Joe Hart.
Phil Brown wa Hull City atobolew mfuko………………!!!!!

Meneja wa Hull City, Phil Brown, amepigwa Faini ya Pauni 2500 na FA, Chama cha Soka England, baada ya kupatikana na hatia ya kutoa maneno ya kashfa dhidi ya Refa Mike Riley.
Sokomoko la Phil Brown lilitokea baada ya Hull City kufungwa 2-1 huko Emirates Stadium kwenye Robo Fainali ya Kombe la FA na Wenyeji Arsenal mwezi Machi na Brown kudai baada ya mechi hawakufungwa na Arsenal bali na Refa Mike Riley na Msaidizi wake walipokubali goli lililofungwa na William Gallas ambalo alidai ni ofsaidi.

No comments:

Powered By Blogger