Thursday 25 June 2009

KIPIGO CHA MAREKANI: SPAIN WASINGIZIA VUVUZELA!!!!!!
Baada ya USA kuibamiza Misri mabao 3-0 siku ya Jumapili kwenye mechi yao ya mwisho ya Kundi lao iliyowafanya USA kutinga Nusu Fainali, Afisa mmoja wa Timu ya Misri alizilaumu taarifa za Vyombo vya Habari huko Afrika Kusini kwamba Timu yake ilikuwa ikizungukwa na MaCD kila wakati na hatimaye kuibiwa pesa ndizo zilizowaathiri na kusababisha wafungwe.
Kwa Xabi Alonso wa Spain, anaechezea Liverpool, VUVUZELA ndilo lililowatibua sana na, kwa yeye, ingekuwa bora kama lingepigwa marufuku uwanjani.
Katika mechi ya jana, kama desturi huko Bondeni, VUVUZELA lilitamba na kupulizwa dakika zote za mechi hiyo iliyowatoa ngebe Spain.

VUVUZELA ni tarumbeta la plastiki na ni kiburudisho mahsusi kwenye mechi huko Bondeni.
Lakini Kocha wa USA, Bob Bradley, amesema mafanikio ya USA yametokana na plani yao ya kuwasimamisha Spain.
Bradley anasema: ‘Spain ni Timu supa lakini tuliamini tutawafunga! Ilibidi tucheze kitimu, tujihami kwa pamoja na tuwe wakali tukishambulia. Kitu kikubwa ilikuwa tusiwape mwanya kwenye Kiungo, tuwakabe kila wakipata mpira na hasa Xavi. Tulihakikisha Xavi hapenyezi pasi zake mbele za kuikata defensi! Tulimlazimisha atoe pasi upande au arudishe nyuma!’
USA wanangoja mshindi wa leo kati ya Afrika Kusini na Brazil kucheza nae Fainali hapo Jumapili.

No comments:

Powered By Blogger