Thursday 25 June 2009

VUVUZELA LAZIMIKA KIUME!!
Ndani ya Ellis Park, Johannesburg, mbele ya Rais Jacob Zuma aliekaa pamoja na Sepp Blatter wa FIFA, VUVUZELA liligoma kunyamaza hadi dakika ya 88 pale Mchezaji wa Akiba, Dani Alvez, alieingizwa kuchukua nafasi ya Santos, kufunga bao kwa frikiki iliyopinda na kumzidi maarifa Kipa Khune na kuwapatia Brazil bao pekee na la ushindi.
Ingawa Brazil walitawala kidogo, Bafana Bafana walipigana kishujaa na kuyazima mashambulizi yote ya vijana wa Samba kwa mtindo wa kujihami Timu nzima na kushambulia Timu nzima.
Ingawa SAMBA imeibuka Ngoma Tamu, hakika VUVUZELA halikuiabisha Afrika.
Brazil itacheza Fainali na USA siku ya Jumapili.
Mechi ya utangulizi siku hiyo hiyo ni ya kutafuta Mshindi wa 3 kati ya Afrika Kusini na Spain.

No comments:

Powered By Blogger