Saturday 27 June 2009

Allardyce kumsaini Van Nistelrooy?
Meneja wa Blackburn Rovers Sam Allardyce anategemea kumchukua Ruud van Nistelrooy kutoka Real Madrid na amepinga wazo kuwa watamsaini Michael Owen kutoka Newcaslte.
Baada ya kumuuza Roque Santa Cruz kwa Manchester City na Matt Derbyshire alieenda Olympiakos ya Ugiriki wiki hii, Sam Allardyce yuko mbioni kuimarisha safu yake ya Mashambulizi.
"Nani alitegema nitampata Anelka nilipokuwa Bolton? Lakini nilimpata!" Allardyce anahoji. "Itakuwa vyema tukimpata Van Nistelrooy!’.
Kuhusu Owen, Allardyce amekataa kufikiria kumchukua na anatamka: ‘Ni tatizo la kuumia mara kwa mara! Nahitaji Straika atakaecheza mechi 30! Hilo halijatokea kwa Owen kwa miaka minne sasa!’
Ronaldo rasmi Real Julai 1!!!
Nyota wa Manchester United Cristiano Ronaldo atakamilisha taratibu za kuhamia Real Madrid hapo Julai 1 baada ya Manchester United na Real Madrid zote, kupitia tovuti zao, kuthibitisha wameshasaini mkataba kati yao.
Real Madrid imesema itamwanua Ronaldo rasmi hapo Julai 6.
Ronaldo ameshasaini mkataba wa miaka 6 na Real Madrid ambao utamfanya awe Mchezaji mwenye mshahara mkubwa sana Klabuni Real.
Uhamisho wake umeigharimu Real Madrid Pauni Milioni 80 ambayo ni rekodi ya dunia kwa uhamisho.
Glen Johnson rasmi Liverpool!!
Liverpool wamethibitisha kuwa Mlinzi wa England Glen Johnson amesaini mkataba wa miaka minne baada ya uhamisho wake kutoka Portsmouth wa Pauni Milioni 17.5 kukumilika.
Johnson alikuwa pia akiwindwa na Klabu yake ya zamani Chelsea na Manchester City lakini mwenyewe ameamua kwenda Liverpool.
Kutua kwa Johnson, ambae ni Beki wa pembeni kulia, kunamletea utata Beki mwingine kwenye nafasi hiyo, Alvaro Arbeloa, na inasemekana huenda akauzwa.
Tevez adai Berbatov ndio amemfanya akatae kubaki Man U!!!
Ingawa Carlos Tevez hajui ni wapi atacheza msimu ujao, amedai kuwa alitambua siku zake hapo Manchester United zilianza kuhesabika pale aliponunuliwa Dimitar Berbatov kutoka Tottenham. Mkataba wa Tevez na Manchester United unaisha rasmi Juni 30 baada ya kuwa hapo kwa miaka miwili kwa mkopo na Klabu za Manchester City na Chelsea ndizo zinamwania huku Klabu nyingine ya tatu ambayo haikutajwa ipo mawindoni pia.
Tevez anasema: ‘Ferguson aliniambia nisiwe na wasiwasi na Berbatov lakini sikufurahi nilipowekwa benchi!’
Ferdinand Bwana Harusi!!!
Nyota wa Manchester United Rio Ferdinand amekodisha ndege maalum ili kuwabeba Familia na Mrafiki zake zaidi ya 100 kuhudhuria harusi yake itakayofanyika huko Visiwa vya Caribbean.
Ferdinand, 30, anamuoa mpenzi wake wa siku nyingi Rebecca Ellison, 29, wikiendi hii.
Wageni waalikwa kwenye Harusi hii ni Wanafamilia tu na baadhi ya Marafiki zake wa zamani wakiwemo kama Mdogo wake Anton anaechezea Sunderland na Wachezaji wa zamani Michael Dubbery na Jody Morris aliekua akichezea Chelsea.
Rio na Rebecca wako pamoja kwa miaka 7 sasa na wanao watoto wa kiume wawili wanaoitwa Lorenz na Tate.

No comments:

Powered By Blogger