Thursday 25 June 2009

VUVUZELA v SAMBA
Wengine wameshasingizia VUVUZELA kuwa ndilo limewakosesha ushindi, lakini, leo kwenye Nusu Fainali ya Kombe la Mabara, VUVUZELA linakutana na Ngoma Ngumu SAMBA!
Brazil, Vigogo wa Soka duniani na Mabingwa Watetezi wa Kombe hili la Mabara, waliwabamiza Mabingwa wa Dunia Italia 3-0 kwenye mechi yao ya mwisho ya Kundi lao.
Brazil wameshinda mechi zao zote za Kundi lao na kufunga jumla ya mabao 10 huku Luis Fabiano akiongoza kwa mabao matatu, Kaka mawili na Maicon, Robinho, Juan na Felipe Melo bao 1 kila mmoja.
Wenyeji Afrika Kusini walifungwa mechi yao ya mwisho ya Kundi lao mabao 2-0 na Spain lakini wametinga Nusu Fainali.
Katika Kundi lao wameshinda mechi moja, kufungwa moja na suluhu moja.
Wamefunga jumla ya mabao mawili na Mfungaji wao pekee wa mabao hayo ni Bernard Parker.
Afrika Kusini na Brazil wamekutana mara mbili tu na zote kashinda Brazil.
JE VUVUZELA na SAMBA NANI LEO ATABWAGA MANYANGA????

No comments:

Powered By Blogger