Tuesday 23 June 2009

FIFA KUMUENZI MARC-VIVIEN FOE FAINALI YA KOMBE LA MABARA
FIFA imetangaza kuwa siku ya Jumapili kabla ya Fainali ya Kombe la Mabara kuanza kutafanyika kumbukumbu maalum ya Kiungo wa Cameroun Marc-Vivien Foe alieanguka na kupoteza fahamu kwenye mechi ya Nusu Fainali ya Kombe la Mabara huko Ufaransa mwaka 2003 na baadae kufariki mara tu alipofikishwa hospitali.
Foe, umri miaka 28, aligundulika kuwa alikuwa na ugonjwa wa moyo.
Rais wa FIFA, Sepp Blatter, amesema: ‘Lilikuwa tukio la kusikitisha na baya sana. Kabla ya Fainali kuanza, timu zote zitasimama katikati ya Uwanja na tutakuwa na ujumbe kwa dunia nzima kuhusu nini kilitokea.’
Siku aliyokufa Foe alikuwa akiichezea Cameroun mechi yake ya 64.
Foe alizichezea Klabu za Manchester City na Racing Lens ya Ufaransa.

Man City imeistaafisha Jezi Namba 23 aliyokuwa akivaa na kwenye Uwanja wao City of Manchester kuna bustani ndogo ya ukumbusho wake.
Klabu ya Racing Lens iliuita mtaa mmoja jirani na Uwanja wao wa Felix Bollaert jina la Foe kama kumuenzi.
Huko kwao Cameroun alipewa mazishi ya kitaifa.
UZI MPYA WA MAN U WAANULIWA!!!
Jezi mpya zinazosemekana zitatumiwa na Mabingwa Manchester United kwa mechi za nyumbani leo zimezagaa kwenye vyombo vya habari na barua pepe za kibiashara.
Jezi hizo [pichani] nyekundu zina ‘V’ nyeusi kifuani na ukosi mweusi na zinafanana na Jezi zilizovaliwa na Manchester United mwaka 1908-9 walipofika Fainali ya Kombe la FA.
Nike, waliotengeneza Jezi hizo, wametangaza kuwa ni za kusherehekea miaka 100 ya Klabu hiyo.
Jezi hizo zinaambatana na bukta nyeupe yenye mstari mwekundu pembeni na stokingi nyeusi zenye ‘V’ nyekundu nyuma.
England chini ya miaka 21 waikwaa Nusu Fainali UEFA!!
Timu ya Taifa ya England ya Vijana chini ya miaka 21, U21, [Under 21] imeingia Nusu Fainali ya Kombe la UEFA la Vijana baada ya kutoka suluhu 1-1 na Timu ya Vijana ya Ujerumani U21 hapo jana katika mechi ya Kundi B.
England wamemaliza Kundi hilo kwa kuwa vinara wakiwa na pointi 7 na Ujerumani, wa pili wakiwa na pointi 5, na wote wanasonga mbele kuingia Nusu Fainali.
Wapinzani wa England kwenye Nusu Fainali watajulikana leo baada ya mechi za Kundi B kumalizika.
Hadi sasa Kundi B linaongozwa na Italia wenye pointi 4, Sweden pointi 3, Serbia pointi 2 na Belarus pointi 1.
Mechi za mwisho za leo za Kundi hilo ni kati ya Serbia v Sweden na Belarus v Italia.
Katika Kundi lake, England ilizifunga Finland 2-1 na Spain 2-0.
Kikosi cha England kilichopo Fainali hizi ni:
Makipa: Joe Hart, Joe Lewis, Scott Loach.
Walinzi: Martin Cranie, Andrew Taylor, Richard Stearman, Nedum Onuoha, Jack Rodwell, James Tomkins, Micah Richards, Michael Mancienne, Kieran Gibbs.
Viungo: Lee Cattermole, James Milner, Craig Gardner, Mark Noble, Adam Johnson, Fabrice Muamba, Andrew Driver, Danny Rose.
Washambuliaji: Gabriel Agbonlahor, Theo Walcott, Frazier Campbell.
NUSU FAINALI zitachezwa tarehe 26 Juni na FAINALI 29 Juni.

No comments:

Powered By Blogger