Monday 22 June 2009

Lippi hajuti, Dunga kicheko, Wachezaji Brazil walizwa Hotelini!!!!
Kocha wa Italia, Marcello Lippi, ametamka hana nia ya kubadilisha Kikosi cha Italia kwa ajili ya Utetezi wao wa Kombe la Dunia mwakani huko Afrika Kusini baada ya kipigo cha jana cha mabao 3-0 walichobebeshwa na Brazil na kubwagwa nje ya Kombe la Mabara huko Afrika Kusini.
Lippi amesema Kikosi ni kizuri ingawa Waandishi waliomhoji walidai Wachezaji ni Wakongwe.
Lippi alijibu: ‘Vijana gani uwalete? Huwezi ukachezesha Wachezaji wadogo wapya 6 au 7 wakati mmoja!’
Miongoni mwa Wakongwe waliocheza ni Nahodha Fabio Cannavaro, mwenye miaka 35, ambae jana alifikisha rekodi ya Paolo Maldini ya kuichezea Italia mechi 126. Lippi aliongeza: ‘Sijuti. Kama kusikitika basi ni kuwa mechi haikuonyesha dunia ile Italia tunayoijua!’
Nae Kocha wa Brazil Dunga amesema: ‘Tumefurahi! Kadri tunavyozidi kukaa pamoja ndio tunaimarika!’
Nusu Fainali ya Kombe la Mabara, Brazil wanapambana na Wenyeji Afrika Kusini inayofundishwa na Kocha kutoka Brazil, Joel Santana. Dunga anasema: ‘Santana ni Kocha anaeheshimika sana Brazil! Lakini hatuchezi na Santana, tunacheza na Afrika Kusini! Ni Timu ngumu na kama Wenyeji, itakuwa ngumu kuwafunga lakini nina imani na Wachezaji wangu!’
Wakati huo huo, Polisi huko Afrika Kusini wanachunguza wizi wa pesa za Mkufunzi wa Viungo wa Brazil na Mchezaji wao Kleber uliofanyika hotelini kwao.

No comments:

Powered By Blogger