Thursday 25 June 2009

Fabregas apandwa mori na Bunduki bila risasi!!!!

Nahodha wa Arsenal, Cesc Fabregas, amezungumzia kuvunjika kwake moyo kwa Klabu yake kutoweza kunyakua Kombe lolote tangu mwaka 2005 na kudai hilo linamtia hasira sana.
Fabregas, anaevumishwa kuwa anataka kurudi kwao Spain kuchezea timu yake ya utotoni Barcelona, amesema: ‘Kukosa Mataji Arsenal ni kitu kinachontia hasira sana! Mwaka huu tulijitutumua kwa nguvu zote lakini hatukufikia kiwango kile kila mtu anachotegemea toka kwa Arsenal! Kama hushindi kitu kila mtu anakuwa na hasira. Miaka minne sasa, tunahitaji Taji turudishe imani!’
Tevez kwenda Man City?
Baada ya kuivua Jezi Nyekundu ya Man U sasa Tevez huenda akavaa Jezi ya Bluu ya Man City na hili limedokezwa na Mshauri wake Mkuu Kia Joorabchian ambae amedokeza kuwa kwa sasa wanatafakari ofa tatu kutoka kwa Man City, Chelsea na Klabu ya tatu ambayo hakuitaja.
Kia Joorabchian, akizungumza kwenye Radio moja huko Argentina, alisikika akisema: ‘Man City ndio wenye nafasi kubwa kwa sababu wanajenga Timu kubwa. Lakini mkataba wa Tevez na Man U unakwisha tarehe 30 Juni na tunauheshimu. Tutajua nini kitatokea baada ya siku 10.’
Wiki iliyokwisha Manchester United ilithibitisha kuwa Tevez anaondoka baada ya kukataa ofa yao.

No comments:

Powered By Blogger