Monday 22 June 2009

Owen kutimka Newcastle!
Michael Owen amethibitisha atahama Timu iliyoporomoka Daraja Newcastle mkataba wake utakapoisha mwishoni mwa mwezi huu.
Owen, 29, alikataa kuongeza mkataba na Newcastle mwanzoni mwa mwaka na ametangaza nia yake kuendelea kucheza Ligi Kuu England badala ya Daraja la chini la Coca Cola ambako ndiko iliko Newcastle sasa.
Owen amesema: 'Sisaini mkataba. Nataka niwe Ligi Kuu au kokote kule kwenye Daraja la juu.’
Owen, anaepata mshahara wa Pauni Laki 1 kwa wiki alihamia Newcastle kutoka Real Madrid mwaka 2005 kwa ada ya Pauni Milioni 16 na kwa sasa atakuwa Mchezaji huru.
Tangu ahamie Newcastle, Owen amekuwa akikumbwa na majeruhi ya mara kwa mara na amecheza mechi 79 na kufunga mabao 30.
Ruud van Nistelrooy ahimiza Wadachi wenzake kutimka Real Madrid!!!
Ruud van Nistelrooy ametamka ni manufaa kwa Timu ya Taifa ya Uholanzi ikiwa wadachi wote waliokuwa Real Madrid watahama hapo.
Kuna taarifa nzito kuwa Real Madrid inataka kuwamwaga wadachi wote hapo Real na inahaha kutafuta Klabu za kuwauza. Wapo wadachi 6 hapo nao ni Van Nistelrooy, Arjen Robben, ­Wesley ­Sneijder, Royston Drenthe, Rafael van der Vaart na Klaas-Jan Huntelaar.
Pamoja na Wadachi hao Wachezaji wengine walio kwenye ‘listi ya mauzo’ ni Javier Saviola, Mahamadou Diarra and Beki wa zamani wa Manchester United Gabriel Heinze.
Ruud van Nistelrooy ametamka: ‘Wachezaji wa Udachi wana malengo makubwa mbele yao, moja likiwa ni kucheza Fainali Kombe la Dunia huko Afrika Kusini 2010! Wakipata ofa Klabu nyingine ni lazima wakubali! Hapa hamna maana kwao!’
Kuhusu hatma yake binafsi, van Nistelrooy, 32, ambae alifanyiwa operesheni ya goti baada ya kuumia vibaya, anasema: ‘Mimi ni tofauti kwani ndio kwanza nimepona goti! Sijui nani atanitaka!’

No comments:

Powered By Blogger