Wednesday 24 June 2009

NI USA FAINALI! SPAIN NJE!!!
Spain, Mabingwa wa Ulaya na Nambari Wani kwenye listi ya FIFA waliocheza mechi 35 bila kufungwa na kuifikia rekodi ya Brazil, leo kwenye mechi ya Nusu Fainali ya Kombe la Mabara Uwanjani Free State, Blomfontein, Afrika Kusini, wametandikwa mabao 2-0 na USA, Timu ambayo wengi tuliidharau.
Mabao ya USA yalifungwa na Altidore dakika ya 27 na Mchezaji anaecheza Fulham, Clint Dempsey, alietunukiwa zawadi ya Mchezaji Bora wa mechi hii, alifunga la pili kwenye dakika ya 74.
USA imekita Fainali na wanasubiri Mshindi wa mechi ya kesho kati ya Brazil na Afrika Kusini.
Spain atacheza na atakaefungwa mechi hiyo ili kupata Mshindi wa 3.
VIKOSI:
Spain: Casillas, Pique, Puyol, David Villa, Xavi, Torres, Fabregas, Capdevila, Alonso,
Ramos, Riera
USA: Howard, Bocanegra, Onyewu, Dempsey, Davies, Donovan, Bradley, Clark, demerit, Altidore, Spector
REFA: Jorge Larrionda [Uruguay]

No comments:

Powered By Blogger