Tuesday 23 June 2009

MAN U YATHIBITISHA JEZI MPYA!!!
Jezi za kuchezea nyumbani za msimu wa 2009/10 zitazinduliwa rasmi wiki ijayo tarehe 1 Julai baada ya Manchester United kuthibitisha taarifa zilizozagaa leo mitandaoni kuzianika Jezi hizo hasa kwa wale Mawakala Wauzaji kupitia tovuti mbalimbali.
Kwa sababu Jezi hizi hazijazinduliwa rasmi zimetangazwa leo huku zikiwa kwenye kivuli ili kuzizuia zisionekane waziwazi.
Klabu ya Man U imesema Jezi hizo ni kuadhimisha miaka 100 ya Old Trafford na mfumo wake ni kama ule uliovaliwa Karne moja iliyopita.
Jezi hizi zitaanza kuonekana rasmi kwenye Timu pale itakapozuru Mashariki ya Mbali kucheza mechi Nchini Malaysia, Indonesia, Korea na China.
Man U wataruka tarehe 16 Julai kuanza ziara hiyo na siku hiyo ndio Jezi zitaanza kuuzwa kwa Washabiki.
Rio Ferdinand amesema: ‘Kudumisha utamaduni wa Klabu ni muhimu. Msimu uliokwisha tulikuwa na Jezi za Bluu ikiwa kumbukumbu ya kutwaa Kombe la Klabu Bingwa Ulaya mwaka 1968 na hizi za sasa ni za miaka 100 ya Klabu! Klabu hii siku zote inajivunia historia yake na sisi Wachezaji tunaskia fahari!’

No comments:

Powered By Blogger