Tuesday 30 June 2009

Vijana Ujerumani Mabingwa wa Ulaya!! Waikung'uta England 4-0!!!
Timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 21 ya Ujerumani jana huko Malmo, Sweden iliibamiza England kwa mabao 4-0 na kutwaa Ubingwa wa Ulaya wa Vijana.
Mpaka mapumziko Ujerumani walikuwa mbele bao 1-0 kwa bao la alilofunga Gonzalo Castro dakika ya 23.
Kipindi cha pili, Ujerumani waliongeza bao 3 zilizofungwa na Ozil dakika ya 48 na mawili kupitia wagner dakika za 79 na 84.
VIKOSI:
Germany: Neuer, Beck, Howedes, Boateng, Boenisch, Hummels, Johnson, Castro, Khedira, Ozil, Wagner.
Akiba: Fromlowitz, Aogo, Ebert, Marin, Schwaab, Grote, Adlung, Ben-Hatira, Schmelzer, Ede, Sippel.
England: Loach, Cranie, Richards, Onuoha, Gibbs, Cattermole, Muamba, Noble, Milner, Walcott, Johnson.
Akiba: Lewis, Taylor, Stearman, Gardner, Rodwell, Tomkins, Mancienne, Driver, Rose.
Refa: Bjorn Kuipers (Holland).

No comments:

Powered By Blogger