Tuesday 15 September 2009

Adebayor ana mashtaka mawili FA, atakiwa kujibu kabla kesho!!!!
Mshambuliaji wa Manchester City, Emmanuel Adebayor, leo amepewa rasmi mashtaka yake mawili kutokana na vitendo vyake katika mechi ya Jumamosi iliyopita ya LIGI KUU kati ya Man City na Arsenal ambayo Man City walishinda 4-2.
Shtaka la kwanza ni la kutaka kumuumiza Robin van Persie kwa makusudi na la pili ni la kuonyesha mwenendo usiokubalika wakati akishangilia goli lake na kwenda kuwachokoza Mashabiki wa Arsenal.
Adebayor amepewa mpaka Jumatano saa 2 usiku saa za bongo kutoa utetezi wake.
Akipatikana na hatia kwa kosa la kutaka kumuumiza van Persie kwa makusudi basi atafungiwa mechi 3 na adhabu hii itaanza mara moja ikimaanisha mechi ya kwanza kuikosa ni ile ya LIGI KUU ya Jumapili pale Man City watakapoenda Old Trafford kukwaana na Mahasimu wao Manchester United.
FA imesema Refa Mark Clattenburg alisema hakuona Adebayor akimtimba van Persie lakini amethibitisha endapo angeliona tukio hilo basi angemtoa Adebayor kwa Kadi Nyekundu.
Adhabu ya kosa la pili, ikiwa atapatikana na hatia, itatangazwa baadae.

No comments:

Powered By Blogger