Monday 14 September 2009

Park apewa Mkataba mpya wa miaka mitatu!!
Kiungo wa Manchester United kutoka Korea Park Ji-sung inasemekana amesaini Mkataba mpya wa miaka mitatu kufuatana na taarifa alizotoa Wakala wake aitwae Kim Jung-Soo.
Park alijiunga na Manchester United mwaka 2005 akitokea Klabu ya PSV Eindhoven na sasa atabaki Old Trafford hadi 2012.
Park ndie Mchezaji wa kwanza kutoka Bara la Asia kucheza Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE alipocheza mechi ya Fainali dhidi ya Barcelona mwezi Mei mwaka huu.
Benki ya Standard Chartered yawa Mfadhili mpya Liverpool
Standard Chartered Bank itakuwa ndio Mfadhili mpya wa Liverpool baada ya kusaini mkataba wa miaka minne utakaoanza Julai mwakani na kumalizika mwishoni mwa msimu wa 2013/14.
Kwa kusaini mkataba huo wenye thamani ya Pauni Milioni 80, Liverpool watatengana na Mfadhili wao mkuu Kampuni ya Bia ya Carlsberg ambae walikuwa nae kwa miaka 17.
Hivi karibuni Manchester United nao walipata Ufadhili mkubwa kutoka Kampuni kubwa ya Kimarekani iitwayo Aon na wao pia mkataba utaanza mwakani.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE KESHO:
[mechi zote saa 3 dak 45 usiku bongo taimu]
Jumanne, 15 Septemba 2009
Atletico Madrid v Apoel Nicosia
Besiktas v Man U
Chelsea v FC Porto
FC Zurich v Real Madrid
Juventus v Bordeaux
Maccabi Haifa v Bayern Munich
Marseille v AC Milan
Wolfsburg v CSKA Moscow
Jumatano, 16 Septemba 2009
Dynamo Kiev v Rubin Kzan
Inter Milan v Barcelona
Liverpool v Debrecen
Lyon v Fiorentina
Olympiakos v AZ Alkmaar
Sevilla v Unirea Urziceni
Standard Liege v Arsenal
VfB Stuttgart v Rangers

No comments:

Powered By Blogger