Sunday 13 September 2009

Kipa wa Besiktas Rustu Recber augwaya Mpira wa Adidas unaotumika Ulaya!!!
Adai unawasaidia sana Washambuliaji kuliko Makipa!!!

Kipa wa Besiktas ya Uturuki, Rustu Recber, ambae alikuwa Kipa nambari wani Timu ya Taifa ya Uturuki, amedai mpira uliotengenezwa na Kampuni ya Adidas unaoitwa ‘Finale 9’ ambao hauna maungio kwani umeumbwa kwa utaalam wa hali ya juu wa kisasa, unawasaidia sana Washambuliaji kwa vile huwezi kutabiri utaruka vipi na kwenda wapi.
Mpira huo ndio utatumika huko Ulaya kwenye mashindano ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Mpira huo ‘Finale 9’ ulitumika kwa mara ya kwanza kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu uliokwisha kati ya Manchester United na FC Barcelona.
Recber amesema: “Tangu 2002 mipira yote iliyotengenezwa na Adidas hubadili spidi na mwelekeo ikiwa hewani baada ya kupigwa shuti! Hii ni ngumu kwa Makipa lakini ni furaha kwa Washambuliaji na UEFA kwani wanataka magoli mengi kuwafurahisha Washabiki!”
Maoni hayo ya Recber yameungwa mkono na Kipa wa Spain anaedakia Real Madrid Iker Casillas.
Besiktas siku ya Jumanne watakuwa wenyeji wa Manchester United kwenye mechi ya kwanza ya Kundi lao kwenye ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

No comments:

Powered By Blogger