Wednesday 16 September 2009

Klabu za LIGI KUU kuwa na Kikosi chenye Wachezaji 25 tu!!
Klabu za Ligi Kuu England zimepiga kura na kukubaliana kuwa kuanzia msimu ujao Klabu zinatakiwa ziwe na Kikosi cha Wachezaji 25 tu na kati yao si zaidi ya Wachezaji 17 wanatakiwa wawe na umri wa zaidi ya miaka 21 na wanaweza kutoka nje ya England na Wales.
Wachezaji wanane kwenye Kikosi hicho cha Wachezaji 25 ni wale waliofundishwa ndani ya Klabu hizo ama popote ndani ya England na Wales na wawe chini ya miaka 21 na wamefunzwa ndani ya England na Wales kwa muda usio chini ya miaka mitatu.
Hata hivyo Klabu zimeruhusiwa kuwa na Wachezaji zaidi ya 25 ili mradi Wachezaji zaidi ya hao 25 wawe na umri chini ya miaka 21.
Kila Klabu inatakiwa kuwasilisha Vikosi vyao mwishoni mwa mwezi Agosti dirisha la uhamisho linapofungwa na wanaweza kuwasilisha tena marekebisho ya Vikosi vyao baada ya kipindi kingine cha uhamisho mwishoni mwa Januari Dirisha la Uhamisho linapofungwa.

No comments:

Powered By Blogger