Monday 14 September 2009

Chelsea yakana madai Abramovich alianguka na kutojiweza akipanda Mlima Kilimanjaro!!!!
Klabu ya Chelsea imekana vikali taarifa kuwa Mmiliki wake Roman Abramovich [pichani akiwa na Kocha Hiddink] alianguka na kutojiweza wakati akipanda Mlima Kilimanjaro Nchini Tanzania wiki iliyopita.
Ilidaiwa kuwa Abramovich alipata matatizo ya kutopumua vizuri alipofika Futi 15,000 juu na hivyo kushindwa kufika kileleni ambako ni zaidi ya Futi 19,000 na kuwaacha baadhi ya watu kwenye msafara wake waendelee juu.
Chelsea imepinga taarifa hizo na pia kusema aliekuwa Kocha wao hivi karibuni Guus Hiddink hakuwamo kwenye msafara huo kama ilivyodaiwa kwani alikuwa Uingereza na Timu ya Taifa ya Urusi, akiwa ndie Kocha wake, iliyocheza na Wales kwenye mechi ya Kombe la Dunia wiki iliyopita.

Klabu ya Chelsea vilevile imekana kuwa Abramovich ilibidi atibiwe na Madaktari kwa matatizo hayo.
Chelsea ilikuwa ikijibu tuhuma zilizozagaa kuwa msafara wake haukujitayarisha vyema hasa kupata uzoefu wa hali ya hewa ya hapo Kilimanjaro na hasa kukabili upungufu wa hewa ya Oksijeni kwenye mwinuko mkubwa.

No comments:

Powered By Blogger