Monday 14 September 2009

POLISI wamlaumu Adebayor kwa fujo za Mashabiki!! Kwa kumpiga buti van Persie huenda akaikosa Man U Jumapili!!
Mshambuliaji wa Manchester City, Emmanuel Adebayor, sasa yuko matatani kwa vitendo vyake viwili alivyovitenda kwenye mechi ya LIGI KUU Jumamosi ambayo Man City waliifunga Arsenal 4-2.
Adebayor alipofunga goli la 3 alikimbia hadi kwa Mashabiki wa Arsenal na kushangilia na Mashabiki hao walipandwa hasira na kutaka kuvamia uwanja lakini Walinzi na Polisi waliokuwepo walidhibiti fujo hizo. Refa Mark Clattenburg alimpa Adebayor Kadi ya Njano kwa kitendo hicho.
Hata hivyo Mlinzi mmoja alijeruhiwa na kupoteza fahamu kwa dakika 5.
Polisi wa Manchester wamesema ni ushangiliaji wa Adebayor ndio uliosababisha fujo hizo na wameliacha suala hilo kwa Man City na FA kuamua nini cha kufanya.
FA imeshatamka inachunguza tukio hilo.
Lakini huenda Adebayor akachukuliwa hatua za haraka na kufungiwa mechi 3 na hivyo kuikosa ‘BIGI MECHI’ ya Manchester kati ya Man U v Man City Jumapili ijayo baada ya Adebayor kumkanyaga usoni Robin van Persie wa Arsenal kitendo ambacho Mchezaji huyo wa Arsenal amesema kilikuwa kusudi ingawa Adebayor anadai ni bahati mbaya na alimwomba radhi van Persie.
Refa hakuona tukio hilo.
LIGI KUU England: Fulham 2 Everton 1
Wakiwa nyumbani uwanjani Craven Cottage, Fulham walijikuta wako nyuma kwa bao 1-0 hadi mapumziko kwa bao la Tim Cahill wa Everton aliloingiza dakika ya 33.
Kipindi cha pili Fulham walikaza buti na kufunga bao mbili kupitia Konchesky dakika ya 57 na Winga Damien Duff aliwapa ushindi dakika ya 79.
Mpaka sasa baada ya mechi 4 Fulham wana pointi 6 na Everton pointi 3.

No comments:

Powered By Blogger