Thursday 17 September 2009

Timu za England zapeta!!! Eto’o, Ibrahimovic ngoma droo!!!
Timu za England zimeendeleza wimbi la ushindi kwenye mechi zao za kwanza kwenye Makundi UEFA CHAMPIONS LEAGUE baada ya Liverpool kushinda 1-0 dhidi ya Debrecen ya Hungary Uwanjani Anfield na Arsenal, waliojikuta wako nyuma 2-0 baada ya dakika 4 tu za mchezo, kuibuka na ushindi wa 3-2 huko Ubelgiji walipokwaana na Standard Liege.
Jumanne, Chelsea na Manchester United zilipata ushindi wa 1-0 kwa kila Timu baada ya Chelsea kuibwaga FC Porto Stamford Bridge na Man U kuishinda Besiktas ugenini Uwanjani Inonu huko Instanbul, Uturuki.
Bao la ushindi kwa Liverpool lilifungwa na David Kuyt baada ya mkwaju wa Torres kutemwa na Kipa wa Debrecen.
Mabao ya Arsenal yalifungwa na Bendtner, Vermaelen na Eduardo.
Katika ‘Bigi Mechi’, huku Dunia nzima ikawakazia macho Washambuliaji Samuel Eto’o wa Inter Milan na Zlatan Ibrahimovic wa FC Barcelona, timu hizo zilitoka suluhu 0-0 zilipocheza nyumbani kwa Inter Milan Uwanjani San Siro.
Kivutio kwa Washambuliaji hao kimekuja baada ya Mastaa hao kubadilishana Timu Eto’o akitoka Barca kwenda Inter na Ibrahimovic toka Inter kwenda Barca.
Ingawa mechi ilitawaliwa na Mabingwa Watetezi Barca na Ibrahimovic kukosa nafasi mbili tatu, matokeo hayo huenda yakawaridhisha Makocha Jose Mourinho wa Inter na Gurdiola wa Barca hasa kwa vile Timu hizi ndizo zinazotegemewa kusonga mbele toka Kundi hili.
MATOKEO KAMILI MECHI ZA UEFA CHAMPIONS LEAGUE:
Jumatano, 16 Septemba 2009
Dynamo Kiev 3 v v Rubin Kazan 1
Inter Milan 0 v Barcelona 0
Liverpool 1 v Debrecen 0
Lyon 1 v Fiorentina 0
Olympiakos 1 v AZ Alkmaar 0
Sevilla 2 v Unirea Urziceni 0
Standard Liege 2 v Arsenal 3
VfB Stuttgart 1 v Rangers 1

MECHI ZIJAZO UEFA CHAMPIONS LEAGUE:
Jumanne, 29 Septemba 2009
AZ Alkmaar v Standard Liege
Arsenal v Olympiakos
Barcelona v Dynamo Kiev
Debrecen v Lyon
Fiorentina v Liverpool
Rangers v Sevilla
Rubin Kazan v Inter Milan
Unirea Urziceni v VfB Stuttgart
Jumatano, 30 Septemba 2009
AC Milan v FC Zurich
Apoel Nicosia v Chelsea
Bayern Munich v Juventus
Bordeaux v Maccabi Haifa
CSKA Moscow v Besiktas
FC Porto v Atletico Madrid
Man U v Wolfsburg
Real Madrid v Marseille
EUROPA LIGI LEO:
[Kuna jumla ya mechi 24 na hapa zinatajwa mechi zinazohusu Timu za Uingereza tu]
Alhamisi, 17 Septemba 2009
Hapoel Tel Aviv FC V Celtic
PFC CSKA Sofia v Fulham
Everton v AEK Athens
LIGI KUU ENGLAND WIKIENDI HII:
[saa za bongo]
Jumamosi, 19 Septemba 2009
[saa 8 dak 45 mchana]
Burnley v Sunderland
[saa 11 jioni]
Bolton v Stoke
Hull v Birmingham
[saa 1 na nusu usiku]
West Ham v Liverpool
Jumapili, 20 Septemba 2009
[saa 9 na nusu mchana]
Man U v Man C
[saa 10 jioni]
Wolves v Fulham
[saa 11 jioni]
Everton v Blackburn
[saa 12 jioni]
Chelsea v Tottenham

No comments:

Powered By Blogger