Sunday 13 September 2009

Tottenham 1 Manchester United 3
Manchester United, Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, jana wakiwa ugenini mjini London Uwanjani White Hart Lane nyumbani kwa Tottenham, timu ambayo ilikuwa haijafungwa hata mechi moja msimu huu wa Ligi, jana mbali ya kujikuta iko nyuma kwa bao 1-0 lilofungwa sekunde ya 51 tangu mechi ianze na Jermaine Defoe na baadae ikijikuta inacheza watu 10 baada ya Mchezaji wao Mkongwe Paul Scholes kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu, ilitoa somo la hali ya juu ya jinsi ‘Soka Bora na Tamu” linavyochezwa.
Baada ya Manchester United kufungwa bao hilo moja walitulia na kutandaza soka la hali ya juu na kusawazisha bao hilo kupitia Mkongwe Ryan Giggs aliefunga kwa frikiki murua ambayo sasa itawafanya Washabiki wake wamsahau mpigaji frikiki wao wa kawaida Cristiano Ronaldo.
Mbrazil Chipukizi Anderson, alieonyesha ukomavu mkuu katika kiungo, aliipatia Man U bao la pili na la kwanza kwake kwenye Ligi Kuu tangu ajiunge Man U.
Hadi mapumziko Tottenham 1 Man U.
Kipindi cha pili ndipo, Paul Scholes, baada ya tayari kuwa na Kadi moja ya Njano, alipewa Kadi ya pili ya Njano baada ya kuonekana amemchezea Rafu Tom Huddlestone ingawa marudio ya video yalionyesha ni Mchezaji wa Spurs ndie aliecheza rafu. Hiyo ilikuwa dakika ya 59 na Scholes akapewa Kadi Nyekundu.
Hata hivyo, dakika ya 79, Wayne Rooney alifunga bao zuri baada ya kuihadaa ngome na Kipa Cudicini wa Spurs.
Tottenham: Cudicini, Corluka, King, Bassong, Assou-Ekotto, Lennon, Huddlestone, Palacios, Defoe, Crouch, Keane. Akiba: Gomes, Hutton, Bentley, Jenas, Pavlyuchenko, Naughton, Kranjcar.
Man Utd: Foster, O'Shea, Ferdinand, Vidic, Evra, Fletcher, Scholes, Anderson, Giggs, Berbatov, Rooney. Akiba: Kuszczak, Owen, Carrick, Nani, Fabio Da Silva, Jonathan Evans, Valencia.
Fergie akerwa na Refa kumtoa Scholes
Sir Alex Ferguson ameeleza kuwa Refa Andre Marriner kumpa Kadi Nyekundu Paul Scholes katika mechi ya jana Manchester United waliyoifunga Tottenham ni kitendo ‘kibaya sana’ na hakikustahili.
Schools alipewa Kadi mbili za Njano, na ya pili ikiwa dakika ya 59 walipovaana na Tom Huddlestone na hivyo kupata hiyo Nyekundu.
Ferguson alilalamika: “Ni makosa kumtoa! Na tungeweza kuathirika, tuko ugenini tunaongoza 2-1 dakika ya 59 na tunabakishwa mtu 10! Hakumgusa! Nimetizama video ile mara 2 na pengine ni Huddlestone aliecheza rafu!”
Van Persie adai Adebayor alimtimba makusudi amuumize!!!
=Adebayor huenda akasulubiwa na FA kwa ushangiliaji!!!
Emmanuel Adebayor, aliefunga bao moja dhidi ya Timu yake ya zamani Arsenal katika mechi ya jana ambayo Manchester City iliipiga Arsenal 4-2, huenda akawa matatani na FA hasa baada ya kufunga goli hilo la 3 na kisha kukimbia nusu ya Uwanja na kwenda mbele ya Mashabiki wa Arsenal kushangilia kitendo ambacho Refa alimpa Kadi ya Njano.
Mashabiki hao wa Arsenal walichukizwa sana na kitendo hicho na ilibidi Polisi na Walinzi wawatulize.
Ndani ya uwanja, Mchezaji wa Arsenal, Robben van Persie amedai Adebayor alimkanyaga usoni makusudi ingawa Adebayor mwenyewe amekiri hilo lakini amesema ni bahati mbaya na alimwomba radhi van Persie.
Kitendo hicho hakikuonekana na Refa lakini van Persie amepinga kuwa Adebayor alimwomba radhi na aliendelea kung’ang’ania alitimbwa kusudi
.

No comments:

Powered By Blogger