Wednesday 16 September 2009

Scholes aipa ushindi Man U ugenini, Anelka aipaisha Chelsea kwao!!
Jana kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE, Klabu za England zilianza vyema kampeni zao za kutwaa Ubingwa wa Ulaya baada ya kushinda mechi zao za kwanza kwenye Makundi huku Manchester United wakishinda bao 1-0, bao lililofungwa na Paul Scholes dakika ya 77, wakiwa ugenini Instanbul, Uturuki walipocheza na Besiktas na Chelsea, wakiwa nyumbani Stamford Bridge, walipata ushindi kupitia Nicolas Anelka goli 1-0 dhidi ya FC Porto ya Ureno.
Leo, Klabu nyingine za England, Arsenal na Liverpool, zitatinga uwanjani kufungua kampeni zao za Ulaya na Liverpool watakuwa nyumbani Anfield kuikaribisha Debrecen ya Hungary wakati Arsenal watasafiri hadi Ubelgiji kucheza na Standard Liege.

MATOKEO KAMILI MECHI ZA JANA:
Atletico Madrid 0 v Apoel Nicosia 0
Besiktas 0 v Man U 1
Chelsea 1 v FC Porto 0
FC Zurich 2 v Real Madrid 5
Juventus 1 v Bordeaux 1
Maccabi Haifa 0 v Bayern Munich 3
Marseille 1 v AC Milan 2
Wolfsburg 3 v CSKA Moscow 1
MECHI ZA LEO Jumatano, 16 Septemba 2009
[saa 3 dak 45 usiku]
Dynamo Kiev v Rubin Kazan
Inter Milan v Barcelona
Liverpool v Debrecen
Lyon v Fiorentina
Olympiakos v AZ Alkmaar
Sevilla v Unirea Urziceni
Standard Liege v Arsenal
VfB Stuttgart v Rangers

No comments:

Powered By Blogger