Tuesday 15 September 2009

UEFA yafuta kifungo cha Eduardo, huru kucheza kesho UEFA CHAMPIONS LEAGUE!!!
Rufaa ya Arsenal waliyokata kwa UEFA kupinga kwa adhabu ya Mshambuliaji wao mwenye asili ya Brazil lakini ni raia wa Croatia, Eduardo, aliyopewa kwa kumhadaa Refa Manuel Gonzalez katika mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE na Celtic hapo Agosti 26, imekubaliwa na UEFA na sasa adhabu ya kufungiwa mechi mbili imefutwa.
Eduardu sasa ni ruksa kucheza mechi ya kesho ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE ugenini Ubelgiji wakati Arsenal watakapokwaana na Standard Liege Uwanja wa Maurice Dufrasne.
Nahodha wa Everton Phillip Neville nje muda mrefu!!
Nahodha wa Everton, Phillip Neville, ambae ni mdogo wake Nahodha wa Manchester United, Gary Neville, atakuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu baada ya kuumia goti walipogongana na Dickson Etuhu wa Fulham katika mechi ya LIGI KUU siku ya Jumapili Uwanjani Craven Cottage na Fulham kushinda 2-1.
Meneja wa Everton David Moyes amethibitisha habari hizo na kusema Neville ataenda kwa Wataalam Jijini London kwa uchunguzi zaidi na hapo ndipo watajua kwa uhakika muda gani atakosekana.
Man City wasubiri litakalomkuta Adebayor!!! Shabiki amlalamikia van Persie Polisi!!
Manchester City wanasubiri kujua hatima ya Mchezaji wao Emmanuel Adebayor kufuatia matukio mawili yanayomhusu yeye yalyotokea kwenye mechi ya LIGI KUU Jumamosi iliyopita ambayo Man City waliifunga Arsenal bao 4-2 Uwanjani City of Manchester.
Tukio la kwanza ni ushangiliaji wa Adebayor alipofunga bao la 3 na kwenda kushangilia mbele ya Washabiki wa Arsenal ambao walikasirika na kutaka kuvamia uwanja lakini wakadhibitiwa na Walinzi pamoja na Polisi.
Katika tukio hilo Mlinzi mmoja alipigwa kichwani na kupoteza fahamu kwa dakika 5 na Polisi wa Manchester wamesema Adebayor ndie chanzo cha fujo hizo.
Refa Mark Clattenburg alimpa Adebayor Kadi ya Njano kwa tukio hilo.
Tukio la pili ni pale Adebayor alipomgusa usoni Robin van Persie kwa buti na ingawa Refa hakuchukua hatua yeyote kwa Adebayor, van Persie alidai Adebayor alikusudia kumuumiza.
Adebayor mwenyewe amekana hilo na kusema alimwomba radhi van Persie ambae amepinga hakuombwa radhi.
FA wanatakiwa kutoa uamuzi kabla ya leo [Jumanne] saa 2 usiku [saa za bongo] kama watachukua hatua zozote kwa Adebayor na baada ya hapo Klabu inapewa masaa 24 kuamua kukata rufaa ikiwa adhabu imetolewa.
Wakati huo huo, ameibuka Shabiki mmoja aliewakilisha malalamiko yake kwa Polisi kuwa van Persie aliwatukana alipokwenda mbele ya Mashabiki wa Man City baada ya kuifungia Arsenal goli dakika ya 62.
Polisi wamesema wanachunguza malalamiko hayo.

No comments:

Powered By Blogger