Saturday 31 October 2009

FIFA U-17 WORLD CUP NIGERIA 2009
Nigeria, Argentina, Uswisi na Mexico zaingia Raundi ya Pili!
Germany na Brazil zasubiri kama zitasonga kwa ushindi wa 3!!!
MATOKEO MECHI ZA Ijumaa, Oktoba 30:
KUNDI A
Germany 3 v Honduras 1
Argentina 1 v Nigeria 2
KUNDI B
Japan 0 v Mexico 2
Switzerland 1 v Brazil 0
Wenyeji Nigeria, baada ya kuanza kwa suluhu mechi yao ya kwanza, hatimaye jana waliifunga Timu ngumu Argentina 2-1 na kuingia Raundi ya Pili kama Washindi wa kwanza wa Kundi lao.
Licha ya kufungwa, Argentina nao wamesonga mbele kama Washindi wa Pili KUNDI A huku Germany anasubiri matokeo ya Makundi mengine ili kujua kama atafaulu kusonga mbele kama mmoja wa Washindi wa Tatu bora wanne.
Katika Kundi B Uswisi na Mexico zimemaliza nafasi za kwanza na za pili na hivyo kusonga mbele na kuwaacha Brazil wakisubiri hatima yao kama Mshindi wa 3.
MECHI ZA LEO Jumamosi, Oktoba 31:
KUNDI C
31/10/09 Gambia v Colombia
31/10/09 Netherlands v Iran
KUNDI D
31/10/09 Burkina Faso v Costa Rica
31/10/09 New Zealand v Turkey

No comments:

Powered By Blogger