Saturday 31 October 2009

KOMBE LA CARLING: DROO YA ROBO FAINALI YATANGAZWA!!
Blackburn v Chelsea
Manchester City v Arsenal
Manchester United v Tottenham
Portsmouth v Aston Villa
Mabingwa Watetezi Manchester United watakuwa wenyeji wa Tottenham kwenye Robo Fainali ya Kombe la Carling, timu ambayo ndiyo waliifunga kwenye Fainali na kutwaa Kombe hilo.
Manchester City watawakaribisha Arsenal City of Manchester Stadium na hii mechi inategemewa kuleta msisimko kwani kwenye mechi ya Ligi Kuu uwanjani hapo mwanzoni mwa msimu ambayo Man City waliikung’uta Arsenal 4-2 vituko vya Mshambuliaji wa Man City, Emmanuel Adebayor, vilizua kasheshe kubwa na kusababisha Mchezaji huyo wa zamani wa Arsenal afungiwe kwa kumtimba Van Persie na kupigwa faini kwa kwenda kuwabeza Washabiki wa Arsenal mara baada ya kufunga goli.
Mechi hizo za Robo Fainali zitachezwa wiki ya kuanzia Novemba 30.

No comments:

Powered By Blogger