Sunday 15 November 2009

KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA: Wajue watakaokuwepo Angola Januari!!
Baada ya mechi za jana kati ya Mataifa mbalimbali ya Afrika zilizotupa Nchi zilizojumuika na Afrika Kusini, Ghana na Ivory Coast kutinga Fainali Kombe la Dunia mwakani huko Afrika Kusini, pia mechi hizo zilituamulia nani atashiriki Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazochezwa huko Angola mwezi Januari, 2010.
Jana Cameroun na Nigeria ziliingia Fainali Kombe la Dunia lakini KUNDI C halikupata Mshindi wa kwenda Fainali hizo baada ya Misri kuifunga Algeria 2-0 na kuzifanya Nchi hizo mbili zilingane kila kitu na hivyo kulazimisha mechi irudiwe Sudan Jumatano ijayo ili kumpata atakaenda Fainali Kombe la Dunia.
Utaratibu uliowekwa ulikuwa Nchi ambayo inamaliza ikiwa nafasi ya Kwanza toka kila Kundi ndio inayoingia Fainali za Kombe la Dunia na zile zinazomaliza nafasi za juu 3 toka kila Kundi zitacheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika pamoja na Mwenyeji Angola.
MSIMAMO TOKA KILA KUNDI:
KUNDI A
-Cameroun pointi 13
-Gabon pointi 9
-Togo pointi 8
-Morocco pointi 3
Kombe la Dunia: Cameroun
Kombe la Afrika: Cameroun, Gabon, Togo
KUNDI B
-Nigeria pointi 12
-Tunisia pointi 11
-Msumbiji pointi 7
-Kenya pointi 3
Kombe la Dunia: Nigeria
Kombe la Afrika: Nigeria, Tunisia, Msumbiji
KUNDI C
-Algeria pointi 13
-Misri pointi 13
-Zambia pointi 5
-Rwanda pointi 2
Kombe la Dunia: Algeria au Misri
Kombe la Afrika: Algeria, Misri, Zambia
KUNDI D
-Ghana pointi 12
-Benin pointi 10
-Mali pointi 8
-Sudan pointi 1
Kombe la Dunia: Ghana
Kombe la Afrika: Ghana, Benin, Mali
KUNDI E
-Ivory Coast pointi 16
-Burkina Faso pointi 12
-Malawi pointi 4
-Guinea pointi 3
Kombe la Dunia: Ivory Coast
Kombe la Afrika: Ivory Coast, Burkina Faso, Malawi

No comments:

Powered By Blogger