Saturday 21 November 2009

LIGI KUU England: Dimbani leo!!
Jumamosi, 21 Novemba 2009 [saa za bongo]
[saa 9 dak 45 mchana]
Liverpool v Man City
[saa 12 jioni]
Birmingham v Fulham
Burnley v Aston Villa
Chelsea v Wolves
Hull City v West Ham
Sunderland v Arsenal
[saa 2 na nusu usiku]
Man U V Everton
Baada ya kutoonekana kwa karibu wiki mbili, leo Uwanjani Anfield, Liverpool wanaikaribisha ‘Timu Tajiri’ Manchester City katika mechi itayoanza mapema kupita zote, itakayoanza saa 9 dakika 45 mchana saa za bongo.
Hii ni mechi ambayo kila upande unataka kushinda kufuatia matokeo mabovu kwao huku Liverpool wakiwa wameshinda mechi 1 tu katika 9 walizocheza mwisho. Mechi ya mwisho ya Ligi Kuu, Liverpool walipata dro 2-2 na Birmingham na wako pointi 11 nyuma ya vinara Chelsea na wameshika nafasi ya 7.
Nao Man City, ingawa wamefungwa mechi moja tu msimu huu kwenye Ligi Kuu, wametoka suluhu mechi 5 zao za mwisho.
Vinara Chelsea wanaikaribisha Wolverhampton Wanderers huko Stamford Bridge na hii inaonekana ni mechi chee kwa Chelsea.
Timu iliyo nafasi ya pili, Arsenal, inasafiri hadi Kaskazini Mashariki na kutua Stadium of Light kucheza na Sunderland huku wakiwa na listi ya majeruhi kibao. Kwenye lisi hiyo wamo Robin van Persie, Clichy na Gibbs.
Hull City na West Ham ni mechi kubwa mno kwa timu hizi mbili na ushindani utazisaidia kujikwamua toka chini.
Mabingwa Manchester United wako nyumbani Old Trafford na wanawakaribisha Everton mechi itakayoanza saa 2 na usiku saa za bongo. Man U ilifungwa 1-0 na Chelsea katika mechi yao ya mwisho na leo wanapambana na Everton ambayo imeishinda Man U mara moja tu katika mechi 28 za Ligi Kuu walizocheza kati yao.
Mechi nyingine za Ligi Kuu leo ni kati ya Birmingham v Fulham na Burnley v Aston Villa.

No comments:

Powered By Blogger