Thursday 19 November 2009

MAGAZETI SWEDEN YAMPONDA REFA WA KWAO WA MECHI YA UFARANSA v IRELAND!!
Magazeti ya Sweden, Nchi anayotoka Refa Martin Hansson [pichani huku Kipa wa Ireland Shay Given akilalamika] aliechezesha mechi ya jana ya Ufaransa v Ireland iliyotoka sare 1-1 na kuwa ‘kipofu’ wakati Thierry Henry akikontroli na kuucheza mpira kwa mkono na kumpasia William Gallas aliefunga bao na kuipa Ufaransa fursa ya kuingia Fainali Kombe la Dunia, yamemponda vibaya Refa huyo wa Sweden.
Gazeti moja la Sweden, Aftonbladet, liliandika: “Kuna takriban Raia wa Ireland Milioni 80 dunia nzima. Tuna uhakika wanajisikia vibaya sana leo! Lakini tunategemea kuna Wasweden watatu ambao watajisikia vibaya mno! Wao ni Refa Martin Hansson na Wasaidizi wake Stefan Wittberg na Fredrik Nilsson! Hamna Fainali za Kombe la Dunia kwa Ireland, lakini tunategemea hata Timu ya Hansson wameifuta haki yao ya kwenda kuchezesha Fainali!!!”

No comments:

Powered By Blogger