Thursday 28 August 2008

ARSENAL WAVUKA KILAINI!!

LIVERPOOL WAINGIA KWA MBINDE!!!

Arsenal wameingia kwenye kapu la droo ya makundi itakayofanyika kesho baada ya kuwazidi kila kitu FC Twente ya Uholanzi kwa mabao 4-0 kwenye Uwanja wa Emirates.
Magoli ya Arsenal yalifungwa na Samir Nasir, Gallas, Walcott na Bendtner.
Arsenal wanasonga mbele kwa jumla ya mabao 6-0.
Liverpool, wakiwa nyumbani Anfield, walihema na kutweta lakini mwishowe walipata bao la ushindi katika muda wa nyongeza dakika ya 118 kwa goli la Dirk Kuyt baada ya kwenda suluhu 0-0 katika dakika 90 za kawaida na hivyo kuwabwaga Standard Liege ya Belgium.
Kesho usiku, saa 1 saa za bongo, kuna droo ya kuchagua timu zipi zinakuwa kwenye makundi.

No comments:

Powered By Blogger