Sunday 24 August 2008

CHELSEA WASIKITISHA...lakini washinda 1-0!!!!
Bao la frikiki ya Mreno Deco kwenye dakika ya nne tu ya mchezo liliwapa Chelsea ushindi finyu wa 1-0 walipocheza na Wigan.
Baada ya goli hilo Wigan wakicheza nyumbani kwao walicharuka lakini walishindwa kurudisha ingawa mafowadi wao Mmisri Amr Zaki na Mwingereza Emile Heskey walihaha kila dakika.
Huu ni ushindi wa pili mfululizo kwa Chelsea baada ya kuwachabanga Portsmouth 4-0 wiki iliyopita wakati Wigan kwao ni kipigo cha pili mfululizo kwani walifungwa 2-1 na West Ham.

No comments:

Powered By Blogger