Saturday 30 August 2008


Manucho akaribia kushuka dimbani na MAN U
Mshambuliaji wa Angola Manucho ambae alisainiwa na Manchester United mwezi Januari mwaka huu kutoka Pedro Atletico ya Angola anakaribia kuvaa jezi ya timu hiyo baada ya kupata rasmi kibali cha kazi nchini Uingereza hivi majuzi ingawa hasa kitu kilicho mchelewesha kuanza kucheza mapema ni kuumia baada ya kuvunjika mfupa kwenye kidole cha mguu wa kulia. Manucho ambae aling’ara sana kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika mwezi Januari akiwa na Timu ya Taifa ya Angola mara baada ya kusaini mkataba na Man U alipelekwa Ugiriki kuchezea timu ya Panathanaikos kwa mkopo ili apate uzoefu na alikuwa na timu hiyo hadi msimu ulipoisha mwezi Mei.
Wadadisi wanahisi Manucho ataliziba vizuri pengo linaloachwa na Louis Saha anaehamia Everton.

No comments:

Powered By Blogger