Tuesday 26 August 2008

RAUNDI YA TATU ya Mtoano ya LIGI YA KLABU BINGWA ULAYA
Mechi za marudiano ya Raundi ya Tatu ya Mtoano ya LIGI YA KLABU BINGWA ULAYA zinachezwa leo na kesho.
Leo ni mechi moja tu kati ya Artmedia na Juventus.
Timu za LIGI KUU UINGEREZA Arsenal na Liverpool zitacheza kesho zote zikiwa viwanja vya nyumbani.
Arsenal alimfunga FC Twente ya Uholanzi kwa bao 2-0 na Liverpool ilitoka sare ya 0-0 na Standard Liege ya Ubelgiji katika mechi ya kwanza.
Washindi wa mechi hizi watajumuika na Mabingwa wa nchi pamoja na timu zilizoshika nafasi ya pili kwenye droo maalum itayofanyika Alhamisi tarehe 28 Agosti ili kupanga Makundi manane ambamo timu zitacheza kwa mtindo wa ligi.

MATOKEO YA MECHI YA KWANZA:
Vitoria Guimaraes 0 v Basel 0
Shakhtar 2 v Dinamo Zagreb 0
Schalke 1 v Atletico Madrid 0
Aalborg 2 v Kaunas 0
Barcelona 4 v Wisla Krakow 0
Levski Sofia 0 v BATE 1
Standard Liege 0 v LIVERPOOL 0
Partizan 2 v Fenerbahce 2
FC Twente 0 v ARSENAL 2
Spartak Moscow 1 v Dinamo Kiev 4
Juventus 4 v Artmedia 0
SK Brann 0 v Marseille 1
Fiorentina 2 v Slavia Prague 0
Galatasaray2 v Steaua Bucharest 2
Sparta Prague 1 v Panathinaikos 2




No comments:

Powered By Blogger