Wednesday 27 August 2008

MCHEZAJI BORA ULAYA KUJULIKANA KESHO!!!!!
-Makundi LIGI ya KLABU BINGWA ULAYA KUPANGWA!
Chama cha Mpira ULAYA, UEFA, kesho Alhamisi tarehe 28 Agosti 2008, kitatangaza washindi wa tuzo mbalimbali za Wachezaji Bora wa Klabu za Ulaya kwa msimu wa 2007/8 na vilevile itafanyika droo maalum ili kupanga Makundi ya Mashindano ya LIGI ya KLABU BINGWA ULAYA ya msimu huu 2008/9 ambayo itaanza tarehe 16 Septemba 2008.
Ijumaa tarehe 29 Agosti 2008, Mabingwa wa LIGI ya KLABU BINGWA ULAYA Manchester United watapambana na Mabingwa wa Kombe la UEFA Zenit St Petersburg ya Urusi kugombea UEFA Super Cup mjini Monaco kwenye Uwanja wa Stade Louis II.
Kati ya Wachezaji 20 waliomo kwenye listi ya mwisho ya Wachezaji Bora, wachezaji 17 wanatoka kwenye Klabu za LIGI KUU UINGEREZA.
Juu ya yote, mmoja kati ya hawa Wachezaji 20 Bora ndie atakaevikwa Taji la Mchezaji Bora wa Klabu wa Ulaya kwa msimu wa 2007/8.
Wachezaji wanaogombea tuzo na nafasi zao pamoja na Klabu watokazo ni kama ifuatavyo:
UEFA KIPA BORA WA MWAKA
-Manuel Almunia [ARSENAL]
-Petr Cech [CHELSEA]
-Manuel Nuer [FC SCHALKE 04]
-Pepe Reina [LIVERPOOL]
-Edwin van der Sar MANCHESTER UNITED]
UEFA MLINZI BORA WA MWAKA
-Jamie Carragher [LIVERPOOL]
-Rio Ferdinand [MANCHESTER UNITED]
-Carles Puyol [FC BARCELONA]
-John Terry [CHELSEA]
-Nemanja Vidic [MANCHESTER UNITED]
UEFA KIUNGO BORA WA MWAKA
-Michael Essien [CHELSEA]
-Cesc Fabregas [ARSENAL]
-Steven Gerrard [LIVERPOOL]
-Frank Lampard [CHELSEA]
-Paul Scholes [MANCHESTER UNITED]
UEFA MSHAMBULIAJI BORA WA MWAKA
-Didier Drogba [CHELSEA]
-Lionel Messi [FC BARCELONA]
-Cristiano Ronaldo [MANCHESTER UNITED]
-Wayne Rooney [MANCHESTER UNITED]
-Fernando Torres LIVERPOOL]

No comments:

Powered By Blogger