Sunday 24 August 2008

Shevchenko arudi AC Milan
Mshambuliaji wa Chelsea Andriy Shevchenko anarudi timu yake ya zamani ya Italia AC Milan kwa makubaliano ambayo yamewekwa siri.
Shevchenko [31] amabae ni raia wa Ukraine alihamia Chelsea mwaka 2006 kutokea AC Milan lakini ameshindwa kutamba kwenye LIGI KUU UINGEREZA ingawa huko AC Milan alikotoka ndie mfungaji anaeshikilia namba mbili katika wafungaji bora wa AC Milan kwenye historia. Alifunga magoli 127 katika mechi 208 alizocheza.
Akiwa Chelsea amefunga goli 9 tu katika mechi 47 alocheza.

DJIBRIL CISSE awaua Spurs!!!

ni mechi yake ya kwanza kwa Sunderland!!!
Mchezaji wa zamani wa Liverpool akichezaji mechi yake ya kwanza tangu ajiunge na Sunderland juzi kwa mkopo kutoka Klabu ya Marseille ya Ufaransa Djibril Cisse alifunga bao la ushindi katikA dakika ya 83 na kuiwezesha Sunderland kuibamiza Tottenham Hotspurs kwa bao 2-1.
Meneja wa Spurs Juande Ramos waliokuwa wakicheza nyumbani kwao Uwanja wa White Hart Lane aliamua kumwacha kwenye timu nyota na mfungaji wao bora Dimitar Berbatov kwa madai kuwa akili yake haijatulia na amekuwa akivuruga maandalizi ya timu kwani mchezaji huyo ameshatoa madai kwa maandishi aruhusiwe kuhamia Manchester United. Mpaka sasa Spurs wamegomea ofa ya Man U kwa mchezaji huyo wakitaka dau lipandishwe.
Awali kwenye dakika ya 55 mchezaji wa zamani wa Man U Kieron Richardson aliipatia Sunderland bao la kuongoza na Nahodha wa Spurs Jermaine Jenas ahasawazisha kwenye dakika ya 73.
TIMU ZILIKUWA:
Tottenham: Gomes, Zokora, King, Woodgate, Assou-Ekotto (Huddlestone 56), Modric, Lennon (Giovanni 56), Jenas, Bentley, Bale, Bent. AKIBA: Cesar, Gilberto, Gunter, Dawson, O’Hara.
Sunderland: Gordon, Bardsley, Nosworthy, Higginbotham, Collins, Malbranque, Whitehead, Reid (Miller 87), Richardson (Cisse 65), Diouf, Murphy. AKIBA: Ward, Chopra, Leadbitter, Healy, Stokes.
WAZAMAJI: 36,064
REFA: Mike Dean (Wirral).

No comments:

Powered By Blogger