Friday 29 August 2008

RONALDO NI BORA ULAYA!!!!!

Cristiano Ronaldo jana alinyakua tuzo mbili za Ulaya, moja ikiwa ni FOWADI BORA ambayo alikabidhiwa na veterani Eusebio na ya pili ni MCHEZAJI BORA ULAYA.
Ronaldo ni mchezaji wa pili wa Manchester United kunyakua tuzo ya MCHEZAJI BORA kwani mwaka 1999 ambapo Man U pia walitwaa ubingwa wa Ulaya David Beckham alishinda tuzo hiyo.
Ronaldo ambae aliwafungia MABINGWA Man U mabao 42 katika msimu wa 2007/8 ndie alikuwa MFUNGAJI BORA wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE kwa kufunga mabao 8.
Tuzo nyingine zilizobaki na kutolewa jana zilinyakuliwa na Wachezaji wa Chelsea. MLINZI BORA ni John Terry, KIUNGO BORA ni Frank Lampard na KIPA BORA ni Petr Cech.

No comments:

Powered By Blogger