Saturday 13 September 2008

ADEBAYOR APIGA GOLI 3!!

Blackburn 0 Arsenal 4

Emmanuel Adebayor aliweka bao 3 mguuni na kuwawezesha Arsenal kushinda mabao 4-0 zidi ya Blackburn katika mechi waliyocheza nyumbani kwa Blackburn kwenye Uwanja wa Ewood Park.
Bao jingine moja la Arsenal alifunga Van Persie.
Katika mechi hii tineja Theo Walcott alikuwa nyota tena kama alivyong'ara Jumatano alipochezea Timu ya Taifa ya Uingereza.
Lakini mechi hii ilipata kivutio pekee pale Bosi wa Arsenal Arsene Wenger alipomuingiza mtoto wa miaka 16 Aaron Ramsey ambae mara baada ya kuingia alimtengenezea pasi supa Adebayor aliefunga bao la nne.

MATOKEO MECHI NYINGINE NI:

FULHAM 2 BOLTON 1,

NEWCASTLE 1 HULL 2,

PORTSMOUTH 2 MIDDLESBROUGH 1,

WEST BROM 3 WEST HAM 2,

WIGAN 1 SUNDERLAND 1,

MAN CITY v CHELSEA kuanza muda si mrefu!!!
Muda si mrefu mechi inayongojewa kwa hamu ambayo ni ya kwanza kwa staa wa Brazil Robinho akichezea timu yake mpya ya Manchester City kwenye Uwanja wa kwao City of Manchester wakipambana na timu inayoongozwa na Mbrazi Luis Felipe Scolari timu ngumu ya Chelsea itaanza.
Matokeo tutawaletea baadae.

No comments:

Powered By Blogger