Saturday 13 September 2008

CHELSEA WAIFUNGA MAN CITY 3-1!

-Nahodha wao John Terry azawadiwa KADI NYEKUNDU!

-Robinho afunga goli la kwanza kwa timu yake mpya Man City!

Katika mechi ya mwisho ya leo ya LIGI KUU UINGEREZA Man City wakicheza nyumbani walifungwa 3-1 na Chelsea.
Robinho akiichezea Man City mechi yake ya kwanza alifunga bao la kwanza la mechi hii na la pekee kwa timu hiyo huku Shaun Wright-Phillips akiwa dhahiri mchezaji bora kwa Man City.
Nahodha wa Chelsea John Terry ambae pia ni Nahodha wa Timu ya Uingereza alipewa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Jo na hivyo ataikosa mechi ya wiki ijayo na Manchester United.

No comments:

Powered By Blogger