Friday 12 September 2008

LIGI KUU UINGEREZA YARUDI DIMBANI KESHO JUMAMOSI!!!!
Baada ya Mechi za kimataifa za kugombea nafasi za kuingia Fainali Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwaka 2010 zilizochezwa wikiendi iliyopita na katikati ya wiki sasa LIGI KUU inarudi tena kesho kwa pambano la watani wa jadi la kukata na shoka kati ya Liverpool na Mabingwa wa LIGI KUU Manchester United mechi itakayochezwa saa 8 dakika 45 mchana saa za bongo Uwanja wa Anfield nyumbani kwa Liverpool.
Wabongo wataiona mechi hii laivu kupitia GTV kwenye chaneli ya GS1.
Mechi hii itakuwa kivutio kikubwa kwani washabiki wengi wana shauku kumuona mchezaji mpya wa Man U Dimitar Berbatov akishirikiana na kina Wayne Rooney na Carlos Tevez kuongoza mashambulizi.
Mechi nyingine inayongojewa kwa hamu ni kumuona mchezaji mpya Robinho wa Manchester City akiikaribisha Chelsea timu aliyoiponda dakika za mwisho na kujiunga Man City badala yake. Pia atakuwemo Shaun Wright-Phillips aliekuwa Chelsea na sasa yuko Man City timu aliyokuwa akicheza kabla ya kwenda huko Chelsea.
Mechi hii iko laivu GTV chaneli ya GS1 kuanzia saa 1 na nusu usiku bongo time.
Wale wapambe wa Arsenal bila shaka watataka kumuona chipukizi wao Theo Walcott akionyesha maajabu yaliyowaua Croatia Jumatano wakati alipochezea Uingereza katika mechi Croatia waliyopigwa 4-1 nyumbani kwao huku bwana mdogo huyu akipachika mabao 3 mguuni kwake.


RATIBA YA MECHI:
JUMAMOSI 13 Septemba 2008
[SAA 8 DAK 45 BONGO TIME]
LIVERPOOL v MAN U
[SAA 11 JIONI BONGO TIME]
BLACKBURN v ARSENAL
FULHAM v BOLTON
NEWCASTLE v HULL
PORTSMOUTH v MIDDLESBROUGH
WEST BROM v WEST HAM
WIGAN v SUNDERLAND
[SAA 1 NA NUSU USIKU BONGO TIME]
MAN CITY v CHELSEA
JUMAPILI 14 Septemba 2008
STOKE CITY v EVERTON
JUMATATU 15 Septemba 2008
TOTTENHAM v ASTON VILLA

No comments:

Powered By Blogger