Monday 8 September 2008

Baada ya Kevin Keagan kutimka, Hughton apewa timu NEWCASTLE!!!
Chris Hughton ameteuliwa kuwa Meneja wa muda wa Newcastle kufuatia kutimka kwa Kevin Keagan aliegombana na Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu hiyo kuhusu kuuza Wachezaji bila kumhusisha.
Vilevile wasaidizi wengine wa Keagan, Terry McDermott na Adam Sadler wameamua kufuata nyayo za bosi wao Keagan na kuamua kuondoka klabuni..
Chris Hughton alikuwa Meneja Msaidizi wa Tottenham kabla ya kuhamia Newcastle msimu uliopita ambako pia alishika wadhifa huohuo.

Hughton atasaidiwa na waliokuwa wasimamizi wa Timu za Vijana hapo klabuni Richard Money na Alan Thompson.
Mechi ya kwanza chini ya usimamizi wa mteule Hughton itakuwa ni wikiendi hii ambako Newcastle watacheza na Hull City.

No comments:

Powered By Blogger