Saturday 13 September 2008

LIVERPOOL 2 MAN U 1 !




Leo Liverpool wameonja ushindi ambao hawajahi kuupata kwa Man U toka Novemba, 2001 wakati mchezaji wao Danny Murphy alipofunga bao moja la penalti!
Mabingwa wa LIGI KUU Man U wakicheza ugenini Uwanja wa Anfield nyumbani kwa Liverpool ndio waliopata bao la kwanza lilofungwa na Carlos Tevez baada ya kazi murua ya Mchezaji mpya Dimitar Berbatov kwenye dakika ya 3.
Liverpool walisawazisha kwa goli la kujifunga mwenyewe la Wes Brown baada ya makosa makubwa ya Kipa Edwin van der Sar wa Man U.
Kipindi cha pili makosa ya Ryan Giggs kutegea mpira utoke yaliwapa mwanya Liverpool kumiliki mpira na Babel akaweka bao la pili.
Beki wa kutegemewa Nemanja Vidic alipewa kadi ya pili ya njano ingawa wengi wanaamini haikustahili na hivyo kulazimika kutoka kwa kadi nyekundu.

No comments:

Powered By Blogger