Wednesday 10 September 2008

ZIDANE ATAMKA: 'RONALDO NI MCHEZAJI BORA DUNIANI!!!'
Aliewahi kuwa MCHEZAJI BORA DUNIANI MARA 3 Zinedine Zidane wa Ufaransa ametamka Cristiano Ronaldo ambae ni staa wa MABINGWA wa UINGEREZA na ULAYA Manchester United ndie pekee anaestahili kuwa MCHEZAJI BORA DUNIANI kwa mwaka 2007/8.
Kwa sasa kuna mjadala mkubwa kuhusu uteuzi wa Mchezaji Bora na unawalenga sana Wachezaji watatu ambao ni Messi, Kaka na Ronaldo.
Msimu uliopita Kaka ndie alieopoa tuzo hiyo.
Ronaldo ambae alifunga jumla ya magoli 42 msimu uliopita kwa sasa yuko nje ya uwanja baada ya kufanyiwa operesheni ya enka na anatarajiwa kurudi dimbani mwishoni mwa mwezi huu.
Ronaldo ndie aliepata tuzo ya MCHEZAJI BORA wa ULAYA pamoja na MFUNGAJI BORA wa ULAYA.
Vilevile amepata tuzo hizo hizo kwenye LIGI KUU UINGEREZA.

No comments:

Powered By Blogger