Tuesday 9 September 2008

FAINALI KOMBE LA DUNIA AFIKA KUSINI 2010

MECHI ZA MCHUJO NCHI ZA ULAYA
Jumatano 10 Septemba 2008
Uingereza kesho itashuka uwanjani mjini Zagreb, Croatia kupambana na timu ya Croatia iliyosababisha isicheze Fainali za EURO 2008 mwaka huu.
Uingereza na Croatia zilikuwa Kundi moja kwenye mashindano hayo na iliifunga Uingereza katika mechi zote mbili za Kundi hilo.
Mechi ya kwanza iliyochezwa nchini Croatia, Uingereza ililamba mabao 3-2 na katika mechi ya pili iliyochezwa Uwanja wa Wembley nyumbani kwa Uingereza, Croatia waliiadhiri vibaya Uingereza walipowashindilia mabao 2-0.
Mechi nyingine inayongojwa kwa hamu ni ya Ufarasa kwani Mabingwa hao wa Dunia wa zamani walitolewa nishai juzi katika mechi ya kwanza ya mchujo huu walipofungwa mabao 3-1 na Austria huko nchini Austria.
Ufaransa atakuwa nyumbani akicheza na Serbia.
MECHI:
Albania v Malta,
Andorra v Belarus,
Azerbaijan v Liechtenstein,
Bosnia-Herzegovina v Estonia,
Croatia v England,
Faroe Islands v Romania,
Finland v Germany,
France v Serbia,
FYR Macedonia v Holland,
Iceland v Scotland,
Italy v Georgia,
Kazakhstan v Ukraine,
Latvia v Greece,
Lithuania v Austria,
Moldova v Israel,
Montenegro v Rep of Ireland,
Northern Ireland v Czech Republic,
Portugal v Denmark,
Russia v Wales,
San Marino v Poland,
Slovenia v Slovakia,
Spain v Armenia,
Sweden v Hungary,
Switzerland v Luxembourg,
Turkey v Belgium,

No comments:

Powered By Blogger