Wednesday 10 September 2008


Zola -huenda leo akapewa Umeneja WEST HAM!

Baada ya kuondoka Meneja Alan Curbishley, West Ham leo inategemewa kumtangaza Mtaliana Gianfranco Zola kuwa Meneja mpya wa klabu hiyo.
Zola ambae alikuwa Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Italy na Chelsea kwa sasa ni Meneja wa Timu ya Taifa ya Italy ya Vijana wa chini ya miaka 21.
Zola ameahidi kuwa endapo atapata fursa hii basi atahakikisa West Ham inacheza aina moja tu ya soka!
Alisema: 'Mie najua kucheza mtindo mmoja tu! Kutuliza mpira chini kwenye kapeti na kushambulia!'

No comments:

Powered By Blogger